![]() |
Yamoto Band |
BAADA ya watu wengi kujiuliza sababu zilizopelekea kundi la Yamoto Band kusambaratika, licha ya kazi nzuri walizokuwa wakifanya, msanii wa bongo fleva katika hilo, Beka Flavour amesema `dogo Aslay' ndio chanzo.
Aslay ambaye alikuwa katika
kundi hilo lililomilikiwa na Saidi fella maarufu `Mkubwa fella' ivi karibuni
ametoa nyimbo tatu zilizokuwa na ujumbe tofauti bila kumshirikisha mtu hata wenzake
waliokuwa kwenye kundi moja.
Beka amefunguka bada ya kuhojiwa katika stori tatu ya Planet bongo ya East
Afrika radio ilifanyika jana kwamba mgogoro ulianza baada ya Aslay kutoa wimbo wa kidawa.
Beka ambaye kwasasa anatamba
na wimbo `Jibebe' ambao ametoa baada ya kusambaratika katika kundi hilo.
Aliendelea kusema Aslay alitoa
wimbo wa `Kidawa' bila hata kumshirikisha mtu yoyote hata viongozi ndani ya
Yamoto.
"Baada ya Aslay kutoa
wimbo wa `Kidawa' kila mmoja alijiona labda hana uwezo wa kuimba ila tulivyoona
hivyo tuliomba kwa uongozi wa Yamoto band ili uturuhusu na sisi tutoe wimbo wa
kujitegemea," amesema.
0 Michango:
Post a Comment