//
Ads

Aishutumu hospitali kumuibia mtoto

Jengo la Hospitali ya Temeke, Dar es Salaam
Na Mwandishi wetu

UTATA umeibuka baada ya Asma Juma, mkazi wa Mbande Kata ya Chamazi jijini Dar es Salaam, kuishutumu Hospitali ya Wilaya ya Temeke kumuibia mtoto mmoja, baada ya kujifungua pacha.
Mwanamke huyo, alisema kabla ya kwenda kupewa rufaa ya kujifungua katika hospitali hiyo, alipima kipimo cha ‘ultrasound’ na kuthibitishiwa kuwa ana mapacha.
Asma alisema awali alikuwa akipata huduma za kliniki katika Zahanati ya Serikali ya Mbande, lakini alikuwa amefanya vipimo vya ‘Ultrasound’ katika Zahanati ya binafsi ya Huruma iliyopo Mbande mara mbili na kuthibitishiwa kuwa ana pacha.
“Wakati napelekwa chumba cha upasuaji nilikuwa sina kichaa cha uzazi, siumwi uchungu, siumwi kichwa, siyo kipofu, siyo kiziwi, nasikia kwa masikio yangu na kumbukumbu zote nimezihifadhi kwenye kichwa changu. Ninachotaka ni mtoto wangu,” alisema Asma.
Mganga Mkuu wa Manispaa ya Temeke, Dk Gwamaka Mwabulambo alikiri kuwapo kwa tuhuma hizo na kusema tayari zinafanyiwa kazi na uongozi.


Source:Mwananchi


Sambaza kwenye Google Plus

Kuhusu Anonymous

Hii ni Blog yenye jukumu la kukupasha habari za Mtanzania mwenye hali ya chini ambaye hajapata nafasi ya kutoa maoni yake.

0 Michango:

Post a Comment