![]() |
Zao la Korosho |
Mwandishi wetu
VIJANA
na wakina mama nchini wametakiwa kujihusisha kwenye sekta ya kilimo cha
biashara ili kujenga uchumi wa kaya zao na Taifa kwa ujumla.
Wito
huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo
Tanzania (TADB) Bwana Francis Assenga wakati akizungumza na waandishi wa habari
jiji Dar es Salaam.
“Vijana na
wamama nchini wanatakiwa kuunda makundi ya Kilimo katika vijiji au kata zao na
kuvisajili ili kuweza kupata mikopo ya riba nafuu kwani kwa kufanya hivyo
kutaongeza Maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla” amesema.
Aidha Bwana Assenga
amesema kuwa kwa makundi yatakayosajili vikundi vyao na kupata mikopo kutoka
Benki ya Kilimo Tanzania, Benki itawasaidia wakulima kupata masoko pasipo
kuhusisha madalali wanaowalaghai na kuwanyonya wakulima pindi wanapouza mazao
yao.
0 Michango:
Post a Comment