//
Ads

Bao la Kichuya laua shabiki wake Taifa

Na Mwandishi Wetu
KLABU ya Simba imepata pigo kwa kuondokewa na shabiki wake, Elius Mweta aliyefariki dunia akiwa uwanjani akishangilia mpira.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, Mweta ambaye ni mkazi wa Kawe, Dar es salaam alifariki baada ya kupata Shinikizo la moyo ghafla wakati akishangilia goli la pili la Simba.

Manara amechukua nafasi hiyo kuwataka wanachama wa Simba katika matawi yao yote kupeperusha bendera zao klabu hiyo nusu mlingoti kama ishara ya kuomboleza kifo cha shabiki mwenzao wa Simba.


Aidha Uongozi wa Simba umeomba wapenzi wa Simba na mpira wa miguu kwa ujumla kujitokeza kesho saa kumi katika mazishi yatakayofanyika Kawe.
Sambaza kwenye Google Plus

Kuhusu Anonymous

Hii ni Blog yenye jukumu la kukupasha habari za Mtanzania mwenye hali ya chini ambaye hajapata nafasi ya kutoa maoni yake.

0 Michango:

Post a Comment