//
Ads

Kebwe akemea vurugu uchaguzi mdogo wa madiwani

 Dk. Steven Kebwe
Na Mwandishi wetu
VYAMA vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi mdogo wa Udiwani katika kata ya Kiwanja cha ndege Manispaa na mkoani morogoro vimetakiwa kudumisha Amani na utulivu.


Akitoa wito kwa uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Januari 22 mwaka huu, Mkuu wa Mkoa huo Dk. Steven Kebwe amesema kuwa mkoa hautavumilia kuona chama chochote kinakiuka masharti ya uchaguzi huo kwa namna yoyote ile.

Dk. Kebwe amewashauri wananchi kuwa watulivu katika kipindi hiki cha Kampeni na kuwataka kusikiliza maelezo yanayotolewa na vyama vyote ili waweze kuchagua kiongozi watakaye muona atafaa kuwaletea maendeleo ya kweli.


Sambaza kwenye Google Plus

Kuhusu Anonymous

Hii ni Blog yenye jukumu la kukupasha habari za Mtanzania mwenye hali ya chini ambaye hajapata nafasi ya kutoa maoni yake.

0 Michango:

Post a Comment