Na Mwandishi wetu
MCHEZAJI nyota wa Ivory Coast Yaya Toure amesema hajapinga shtaka la kuendesha gari akiwa amelewa wiki mbili zilizopita.
Hata hivyo,
amesema kwamba hakunywa pombe makusudi alipokamatwa akiendesha gari akiwa
mlevi.
Ameandika kwenye
Facebook kwamba "inafahamika wazi kwamba mimi ni Mwislamu na huwa sinywi
pombe."
Hata hivyo,
hajaelewa ni vipi alijipata akinywa pombe ama akajipata akiwa amelewa bila yeye
kufahamu.
Yaya Toure aomba
msamaha Man City
Yaya Toure: Uamuzi wa Fifa utawaumiza wachezaji
Mchezaji huyo wa Manchester City amesema: "Daima nimekuwa nikikataa pombe. Yeyote anayenifahamu na anayefuatilia uchezaji wangu atakuwa bila shaka ameniona nikikataa shampeni ya Mchezaji Bora wa Mechi kwa sababu ya kujitolea kwangu kuheshimu dini yangu."
Yaya Toure: Uamuzi wa Fifa utawaumiza wachezaji
Mchezaji huyo wa Manchester City amesema: "Daima nimekuwa nikikataa pombe. Yeyote anayenifahamu na anayefuatilia uchezaji wangu atakuwa bila shaka ameniona nikikataa shampeni ya Mchezaji Bora wa Mechi kwa sababu ya kujitolea kwangu kuheshimu dini yangu."
"Ni muhimu
kwangu kwamba niliiambia mahakama kwamba sikunywa pombe makusudi. Jaji
akinihukumu mwenye alikubali kwamba sikuwa nimekunywa pombe makusudi."
Amesema kesi yake
ilihitimishwa Jumatatu na kwamba alikubali shtaka.
"Kuendesha gari ukiwa mlevi ni kosa kubwa na ingawa sikunywa pombe makusudi, nakubali marufuku na faini na naomba radhi kwa yaliyotokea," aliongeza.
"Kuendesha gari ukiwa mlevi ni kosa kubwa na ingawa sikunywa pombe makusudi, nakubali marufuku na faini na naomba radhi kwa yaliyotokea," aliongeza.
0 Michango:
Post a Comment