//
Ads

Afande Sele: Najivua ACT, nitabaki kuwa raia wa kawaida

Selemani Msindi (Afande Sele)
Na Mwandishi Wetu
SELEMANI Msindi (Afande Sele) msanii mkongwe wa muziki wa Hip hop hapa nchini na aliyejikita katika masuala ya siasa baada ya kugombea ubunge Morogoro mjini katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana kupitia tiketi ya ACT Wazalendo ametangaza kujivua chama hicho.

Uamuzi wa Afande Sele unakuja ikiwa ni wiki moja tangu Habib Mchange, mmoja kati ya waasisi wa chama hicho atangaze kujivua uanachama wa chama hicho na kuahidi kubaki kama mtanzania asiye na chama.

Ujumbe alioandika Afande Sele kupitia mtandao wa Facebook...

“Leo natangaza rasmi kujivua uanachama wa chama cha ACT-Wazalendo na sitakua mfuasi wa chama chochote cha siasa bali nitabaki kuwa raia wa kawaida ndani ya nchi yetu nikiendelea na majukumu mengine ya kimaisha mpaka nitakavyoamua vinginevyo,” amesema Afande Sele.

Hivi karibuni Afande Sele aliwahi kueleza kutoridhishwa na viongozi wa ACT, akidai wamekuwa vigeugeu kiasi cha kumfanya ashindwe kujua iwapo msimamo wa chama hicho ni kuunga mkono upinzani au chama tawala (CCM).


Sambaza kwenye Google Plus

Kuhusu Anonymous

Hii ni Blog yenye jukumu la kukupasha habari za Mtanzania mwenye hali ya chini ambaye hajapata nafasi ya kutoa maoni yake.

0 Michango:

Post a Comment