//
Ads

Lukuvi avuruga dili la Makonda Kigamboni


Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (mwenye kofia) akiangalia ramani ya ardhi hiyo aliyopewa wiki iliyopita. Picha ndogo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi.

Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ameingiria kati mpango wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kukabidhiwa ardhi kwa ajili ya kujenga viwanda, kwani alidanganywa na aliyempatia.

Lukuvi amesema Makonda alidanganywa na mfanyabiashara, Mohamed Ikbar kuwa ardhi hiyo ni mali yake, huku akijua kuwa ni mali ya serikali.

Makonda (katikati) akikagua ardhi aliyopewa. Kulia mfanyabiashara, Mohamed Ikbar

Waziri huyo amesema serikali itachukua hatua kali za kisheria dhidi ya mfanyabiashara huyo kwani alifanya kitendo hicho makusudi kwa malengo yake binafsi.


"Sitaki ardhi itumike kama sehemu ya wafanyabiashara kutakatisha fedha chafu" amesema Lukuvi.
Sambaza kwenye Google Plus

Kuhusu Anonymous

Hii ni Blog yenye jukumu la kukupasha habari za Mtanzania mwenye hali ya chini ambaye hajapata nafasi ya kutoa maoni yake.

0 Michango:

Post a Comment