Barua ya msomaji
MWAKA 2010 baada ya zoezi la kufungiwa mabomba ya mchina
kupitia kampuni ya Dawasco kukamilika hapa Mlandizi wilayani Kibaha Mkoani Pwani tulitakiwa kulipia huduma hiyo Tsh 5000
kwa kila mwezi.
Malipo yalitakiwa kufanyika bila kuangalia ni wingi gani wa
maji mtumiaji ametumia yaani haikujalisha umetumia maji mengi au machache
malipo yalitakiwa yawe hivyo.
Wananchi tulikubaliana na hilo lakini baada ya miezi michache
huku wakitueleza kuwa tuendelee kusubiri kila mtu aanze kulipia kiwango husika
tukaletewa bili zinazoonesha kwamba miezi yote tuliyolipa pesa haikuwafikia ndipo tukawa tunaendelea kuandikiwa kwamba tuna madeni kila wanapoleta bili zao za mwisho wa mwezi.
Tulitakiwa kulipa madeni hayo na tukalipa lakini bado tunaumizwa na kuambiwa kuwa bado tunadaiwa wakati tumeshalipa na kwamba miamala tuliyoitumia kulipa bado hawaitambui jana tulikutana na Mbunge tukamkumbusha hilo mbunge wa Kibaha Vijijini, Abuu Juma akasema
tumuone mtu anayeitwa Eliudi katika ofisi za Dawasco.
Nilitoka kama mmoja wa wahanga kufuatilia suala hilo, nilionana
naye kumueleza na kumuonyesha ile kalatasi alipoiangalia adai haina saini
na nilipojaribu kumuonesha akasema yeye sio muhusika.
Nilimuona mtu anayehusika na pesa huko sikupata
ufumbuzi wa jambo langu baadae nilipohoji alikuwa dada mmoja naye ni mfanya
kazi akaniambi kwamba nimeshaibiwa na sina wa kumshitaki maana huyo niliyekuwa nampatia
pesa simjui na kwamba nikaandike barua ya madai.
Sasa ninashindwa kuelewa kama ofisi inamwajili
mfanya kazi apokee malipo ya wateja halafu pesa hizo zisemwe hazikufika?
Inawezekanaje wasiwe na kumbukumbu wakati tulikua tunalipa
pesa hizo ofisini hapo na wakipokea pesa wanao pokea wanasaini na kudaiwa
mteja hapa kuna tatizo la kulinda masilahi ya watu na kutuibia sisi
walala hoi naomba itumwe tume ya uchunguzi watusaidie swala hili
kuna majipu hapa dawasa Mlandizi jamani.
Ni mimi
Abdallah Ally, Mlandizi
0 Michango:
Post a Comment