//
Ads

Picha bora zilizopigwa Afrika

Tazama baadhi ya picha bora kutoka barani Afrika na zile za Waafrika wakiwa sehemu mbali mbali duniani.
Mchuuzi awauzia wapita njia na wenye magari panya waliochomwa eneo la Salima, malawi siku ya jumatatu. Panya waliochomwa wanapendwa sana na watu nchini Malawi na biashara yake imenoga sana hasa vijijini.
Mchuuzi akiwauzia wapita njia na wenye magari panya waliochomwa eneo la Salima, Malawi, siku ya Jumatatu. Panya waliochomwa wanapendwa sana na watu nchini Malawi na biashara yake hunoga sana hasa vijijini.

Mwendeshaji pikipiki wa motocross afanya sarakasi katika sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya kuwepo kwa jimbo la Lagos, nchini Nigeria, tarehe 13 Mei, 2017.
Siku hiyo hiyo mwendeshaji pikipiki wa mashindano ya pikipiki wa Afrika Kusini aliwatumbuiza watu waliofika kwenye sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya kuwepo kwa jimbo la Lagos, nchini Nigeria.
Kobe huyo aina ya 'ploughshare' alifikishwa mbele ya wanahabari karibu na uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur huko Sepang, Malaysia. Kobe hao 330 walikuwa wamewekwa kwenye masanduku amabayo yalidhaniwa kusafirisha mawe kutoka uwanja wa ndege wa Antananarivo, nchini Madagascar.
Siku hiyo hiyo kobe huyu wa aina ya 'ploughshare' aliokolewa nchini Malaysia baada ya kusafirishwa kinyemela kutoka Madagascar. Maafisa walipata kobe 330. Kobe hao walikuwa wamewekwa kwenye masanduku amabayo yalidhaniwa kusafirisha mawe kutoka uwanja wa ndege wa Antananarivo, nchini Madagascar.
Sambaza kwenye Google Plus

Kuhusu Anonymous

Hii ni Blog yenye jukumu la kukupasha habari za Mtanzania mwenye hali ya chini ambaye hajapata nafasi ya kutoa maoni yake.

0 Michango:

Post a Comment