//
Ads

Jenerali ulimwengu aungana na Mbowe, kesi ya Makonda

Jenerali Ulimwengu

Na Mwandishi wetu
Katika Kesi hiyo namba moja ya 2017 ambapo Ulimwengu atapeleka Maombi hayo Kesho Mahakama Kuu na kuomba kuwa Mdai kama Mbowe zidi ya Makonda, Kamanda Wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam na Mkuu wa upepelezi Cammillius Wambura.JENERALI Ulimwengu Mwanahabari nguli nchini ameomba kujiunga katika kwenye kesi iliyofunguliwa na Freeman Mbowe mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (Chadema) zidi Paul Makonda Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Awali upande wa wajibu maombi ambao ni Jamhuri waliwasilisha hoja pingamizi ambapo Mwanasheri Mkuu wa Serikali Gabriel  Malata alidai kuwa maombi hayo yameletwa chini ya sheria isiyotakiwa na kwamba hayana mashiko. Malata alidai maombi hayo yameletwa nje ya muda kwa kuwa tayari Mbowe alikamatwa, alifanyiwa mahojiano na aliachiwa na Polisi.

‘Hati ya kiapo cha mdai (Mbowe) ina mapungufu kwa sababu kwa mujibu wa sheria kiapo kinatakiwa kielezee facts (maelezo) na sio mawazo ya mtu hivyo sio sahihi tunaomba maombi haya yatupiliwe mbali kwa gharama ya kesi,’’ alidai Malata.

Pia alidai kuwa kiapo hicho ndio kinabeba maombi ya mdai hivyo yakiwa na mapungufu hata maombi yake yanakuwa na mapungufu.

Malata alidai maombi hayo yanahusiana na kesi za jinai na kwamba Mahakama Kuu haina mamlaka ya kutoa maamuzi yanayohusiana na jinai hivyo, wadai walipaswa kupeleka kesi hiyo katika mahakama husika.

Akijibu mapingamizi hayo, Wakili Kibatala alidai kuwa mwanasheria wa serikali alitakiwa kuonesha ni kifungu gani cha sheria ambacho kingeiongoza mahakama katika njia sahihi kuhusu maombi hayo.

Pia alidai kuwa sheria iliyotumika kufungulia maombi hayo iko sahihi hivyo kungekuwa na mapungufu upande wa wadaiwa ungeonesha ni sheria ipi.

Hata hivyo, katika hoja ya kuingizwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) katika kesi hiyo liliibuliwa lakini mahakama iliamuru upande wa wadai urekebisha maombi yao kwa kuwa hawakumuingiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) licha ya kuishitaki serikali.

“Tutafanya marekebisho ya maombi yetu na marekebisho mengine madogo madogo kwa namna tutakavyoona inafaa siku ya jumatatu na tutawapa wajibu maombi Machi 6, mwaka huu na Machi 8, mwaka huu itatajwa kwa ajili ya kusikiliza maombi hayo,” alidai Lissu.

Katika kesi ya msingi, Mbowe anaomba mahakama iwazuie wadaiwa kutekeleza azma yake ya kumtia mbaroni pia itoe amri ya kuwazuia kumkamata hadi hapo kesi hiyo ya kikatiba itakapomalizika na kwamba polisi wasiendelee na mchakato wowote dhidi yake hadi hapo kesi hiyo itakapomalizika.

Anadai kuwa sheria inayompa Mkuu wa Mkoa mamlaka ya kutoa amri ya kumkamata na kumweka ndani mtu iko kinyume cha katiba, kwa madai kuwa ilitungwa katika mazingira ambayo hapakuwa na vituo vya polisi vya kutosha. Pia anadai kuwa kwa mazingira ya sasa sheria hiyo imeshapitwa na wakati na anaiomba mahakama itamke kuwa ni kinyume cha katiba.

Mbowe pia anadai kuwa hata kama Mkuu wa Mkoa alikuwa anatekeleza mamlaka yake kwa mujibu wa sheria hiyo basi hakutimiza matakwa ya kisheria, ambayo ni pamoja na kutoa taarifa kwa Hakimu wa Mahakama ya Wilaya au ya Hakimu Mkazi.

  Kesi hiyo itaendele Tarehe 3 Mwezi Machi mwaka huu.


Sambaza kwenye Google Plus

Kuhusu Anonymous

Hii ni Blog yenye jukumu la kukupasha habari za Mtanzania mwenye hali ya chini ambaye hajapata nafasi ya kutoa maoni yake.

0 Michango:

Post a Comment